Mjadala mkali umeibuka mtandaoni baada ya picha za Tiffah, binti wa Diamond Platnumz, kuonekana akiwa amevaa kikuku mguuni. Watu wamekuwa na maoni tofauti kuhusu maana na umuhimu wa mapambo hayo kwa watoto.
Hii si mara ya kwanza kwa familia ya Diamond kuzua gumzo kuhusu kikuku. Mnamo 2018, Diamond mwenyewe alikumbwa na mjadala kama huu baada ya kuonekana akivaa kikuku, akisisitiza kuwa ni suala la mtazamo wa kitamaduni na mtu hawezi kupangiwa avae nini.